Droo ya michuano ya UEFA yakamilika timu za Uingereza hali tete, Zidane uso kwa uso na Guardiola
Droo ya michuano ya UEFA yakamilika timu za Uingereza hali tete, Zidane uso kwa uso na Guardiola
Droo iliyokuwa ikisubiriwa kwa ham sana ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya UEFA tayari imekamikilika na kila timu imemfahamu mpinzania wake.
Katika moja ya timu iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu sana Liverpool ikiwa kama bingwa mtetezi imepangiwa na timu moja ya Uhispania ambayo ni Atletico Madrid lakini pia timu nyingine ya Uingereza iliyopangiwa timu kutoka Uhispania ni Manchester City wakipangiwa na mabingwa wa michuano hiyo wa kihistoria Real Madrid.
Mbali na hizo Chelsea pia imepangiwa timu kutoka Ujerumani ambayo ni tishio sana ambayo iliifunga timu kutoka Uingereza Tottenham kwa jumla ya goli 10 kwa 3 kwa mchezo wa kwanza ambao ulifanyika London Baryen Munich iliibuka na ushindi wa goli 7-2 na mchezo wa pili ikiibuka na ushindi wa goli 3-1.
#Bongo5Updates Hivi ndivyo drow ya 16 bora michuano ya UEFA Champions League ilivyoenda na kila timu imemfahamu mpinzani wake:
Kwa mtazamo wako timu gani imeonewa pic.twitter.com/bg0rFYYZMe— bongo5.com (@bongofive) December 16, 2019
By Ally Juma.