Michezo
Emmanuel Eboue kurejea Ligi Kuu ya England
Beki wa kimataifa wa Ivory Coast, Emmanuel Eboue anategenea kurejea tena katika Ligi Kuu ya England baada ya klabu ya Sunderland inatarajiwa kumsajili beki huyo wa zamani wa Galatasaray, Emmanuel Eboue kwa mkataba wa hadi mwishoni mwa msimu.
Beki huyo wa zamani wa Arsenal amekuwa kivutio kwenye mazoezi ya Sunderland na leo anatarajiwa kusaini Mkataba wa hadi mwishoni mwa msimu.
Eboue mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kutemwa na klabu ya Galatasaray mwaka jana. Kwa wiki tatu amekuwa akifanya mazoezi na Sunderland na akacheza dakika zote 90 Jumatatu U21 ya klabu hiyo ikiifunga Leicester City.