Burudani

Fid Q adai views za YouTube siyo ishu

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Fid Q amedai idadi ya views katika mtandao wa YouTube si kipimo katika muziki wa hip hop Bongo.

Rapper huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma zake mbili mpya ‘Fresh na Ulimi Mbili’, ameiambia FNL ya EATV kuwa idadi ya viewers mara myimgi huenda kinyume na uhalisia.

“Kwanza nafikiri nyingi hazipati (views) hizo kwa sababu wana hip hop ni watu ambao huwa tunatoa ngoma na zinakuwa zimefika. Unajua views na mambo ya YouTube sometimes hayamati sana katika uhalisia, huwa tunakutana na watu ambao wana-views milioni na kadhalika katika show na tunakuwa kama sisi ndio tuna hizi views milioni,” amesema na kuongeza.

“Kwa hiyo huwa nawaambia watu kila siku kwamba number do lie sometime, kwa sababu unaambia mbili jumlisha mbili ni nne na mbili mara mbili ni nne lakini mbili toa mbili ni sifuri,” amesisitiza.

Ngoma mpya Fid Q ‘Fresh’ ambayo aliitoa August 13 mwaka huu hadi sasa ina views 160,646 katika mtandao wa Youtube.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents