JEURI YA PESA: Diamond kutumia mil. 150 kwenye Birthday ya Tiffah, Harmonize akifanya ‘shopping’ ya mil. 100 Afrika Kusini
Kwa sasa ukizungumzia wasanii wenye fedha nchini Tanzania huwezi kuacha kuwataja Harmonize na Diamond Platnumz, na hili linaonekana wazi hata kwenye matumizi yao ya kawaida.
Siku za hivi karibuni Diamond Platnumz ametangaza kuwapeleka watu 50 kutoka Tanzania kwenda Afrika Kusini ambapo kati ya watu hao 30 ni mashabiki wake na 10 watakuwa ni wanakamati wa tukio ambao wataongozana na watoto wao.
Anyway! tupige mahesabu ya kawaida ya nauli ya mtu mmoja ya kwenda Afrika Kusini na kurudi kwa ndege. Kwa nauli ya chini ya daraja la Economy ni dola $600 sawa na tsh milioni 1.350.000.
Ambapo ukizidisha kwa watu 50 utapata milioni 67.5. Gharama za kuishi Afrika Kusini kwa siku tatu kwa watu 50 yaani kuanzia tarehe 17 hadi 19, 2018 kwa hoteli ya bei ya chini ni dola $150 kwa siku ambapo kila mtu kwa siku tatu atatumia dola $450 kwa ajili ya malazi, ambayo ni sawa na tsh 1.2 .
Ukipiga mahesabu ya kawaida ya kila mtu milioni 1.2 ya malazi kwa watu 50 unapata kama tsh milioni 60 na hapo bila gharama ya chakula. So roughly kuwagharamia watu 50, Diamond atatumia si chini ya milioni 150 kwa fedha ya kitanzania ili kukamilisha zoezi la kuwasafirisha watu 150 .
Wakati hayo yakijiri, msanii mwingine kutoka WCB, Harmonize yeye ameonekana akitumia fedha zake kwa matumizi mengine kabisa ikiwemo kununua nguo kutoka kwenye Clothing brand za gharama ya juu kabisa.
Harmonize unaweza ukasema ndio msanii kwa sasa Tanzania ambaye anafululiza kuvaa bidhaa za Gucci ambazo ni moja ya bidhaa za nguo zenye gharama kubwa duniani.
Tuanzie hapa! mwezi uliopita Harmonize alifanya shopping kwenye duka kubwa la bidhaa za Gucci nchini Afrika Kusini ambapo kwa kawaida hauwezi kuingia kwenye maduka hayo ya bidhaa za bei ghali duniani kama hauna dola $30,000 yaani zaidi ya tsh milioni 60.
Hii ndio maana hata baada ya kutoka kwenye duka hilo Harmonize mwenyewe alikiri kuwa bidhaa zao ni ghali sana ingawaje, ndio bidhaa azipendazo sana.
Tuanze na mahesabu ya kawaida kwa nguo alizonunua Harmonize kutoka Gucci, ambazo anazivaa kwa sasa hivi kwenye show yake.
T-shirt kama hiyo unayoiona ameivaa Harmonize kwenye picha akitumbuiza inauzwa kwa dola $980 ambayo ni sawa na Tsh milioni 2.2 za kitanzania.
Soksi za Gucci alizovaa Harmonize kwenye hiyo picha zinauzwa dola $120 kwa pea moja ambayo ni sawa na tsh 273,000/= .
Viatu vya Gucci alivyovaa kwenye hii picha vinauzwa dola $650 ambayo ni sawa na Tsh milioni 1.4, Track suti full ni dola $1,490 ambayo ni sawa na Tsh milioni 3.3 .
Kwa maana hiyo picha hiyo unayoiona juu Harmonize akitumbuiza mavazi yake kwa ujumla ni dola $2,260 ukijumlisha na saa ambayo inauzwa dola $1,020 unapata dola $3,280 ambayo ni sawa na tsh milioni 7.4 .
.
Ukweli ni kwamba Harmonize hana nguo moja au mbili za Gucci kwani karibia show zake zote huwa anabadilisha mavazi hivyo ni uhakika kuwa kwa sasa huenda akawa ni moja ya wasanii wanaovaa nguo za bei ghali zaidi ila sio kupendeza ukimtoa Diamond Platnumz.
Narudia tena Harmonize ni moja ya wasanii wanaovaa nguo za bei ghali zaidi nchini Tanzania ila sio msanii anayependeza zaidi kwani kuvaa kitu cha gharama sio ndio kupendeza.
Faida ya kuvaa nguo hizo za gharama zaidi duniani kwa yeye kama msanii:
Bila ubishi kwa msanii kuvaa nguo za brand za bei kubwa kama Gucci, Louis Vuitton, Chanel, Versace, Balmain, Dolce and Gabbana na Hermès ni moja ya njia ya kujibrand hususani kwa wasanii wa Afrika.
Hujawahi kufikiria, labda P. Diddy amekutana na Harmonize halafu kamkuta na muonekano huo akiwa ametupia bidhaa za Gucci bila shaka utambulisho wake utakuwa wa maana zaidi.
Pia ni status kwa msanii kuvaa nguo ambazo ni nadra kuwakuta watu wa kawaida wakiwa wamevaa, kumbuka utofauti wa muonekano wa kimavazi ni muhimu sana kwa wasanii.
Bei zote zilizotajwa hapo juu ni kwa mujibu wa mtandao wa gucci.com ambapo hazishuki wala kupanda duniani .kote.
Uyo harmonize angekua nayo hyo milion Mia c angeenda kumjengea bibi yake nyumba mtwara uko achen kupaisha watu wakt hawajawa na uwezo huo…shopping milion Mia NAKOJOA. ..HARMO HUYU TUNAEMJUA? ?
Alimuahd noah shilole mpaka leo kimyaaa misifa tu. …
WATU MAPOVU YANAWATOKA KISA M250
Mziki upo wcb ela zpo wcb kiki zko wcb collabo zpo wcb tv pendwa iko wcb mpaka ww unaye comment iyo abari ni ya wcb awa sio watu kweli vile ni majin amien tu
Mmh
aitishi bhana
Basidei zipo tu kwa mwanadam haziishi ukiziendea pupa zita kuumiza.
kanuni ya pesa ukipata fanya kitu cha maana ikikuacha utaisaka usiku na mchana uipati pesa sinchi sana izo
Maisha ni haya hkn mngn
Salut kwenu wcb kweli mmewashaa
Mmeziona izo mill 100
Harmonize si ako mombasa kenya shopping kaifanya lini?
Time will remind him such joke
Pw
Pw
Malk Dosh sio ajab sna kwasabab hata saa anayovaa inagharama ya mil200
Ha ha ha , kumbe kuna ndugu wa Floyd my weather co
Let money speaks, ila tuache uongo vijana wanaztafta
Hahaaa millions what ??
Labda ya kuchora
Kama uwezo upo Fanya shida kuvunja Sheria au?
#masonic_money!!!!!
#wtf
Hebu achen uongo wa kijinga nyie
Yani unacho kisema Ni sahihi awa wajama sio pesa ya kawaida kiukweli ninashaka nao
Bdo unabish tu duuuh binadamu na chuki
Wcb ndo sehemu yakutafutia dunia kama watak dunia omba uingiy wcb utapata awa wajama wanatish sna
Ya dunian wameshapasii
Huo ni uchz.co kua na pesa
Pesa zake hazituhusu wacha tu afanye atakavyo
Kwann unashaka
Naona na one 👃 nose kwa madiba
kashapewa NOAH…..
umaskini mbaya mno
Safi sana,Wcb Hamna Afrc
Watapata tabusana
Saa milioni miambili, shopping milioni Mia duhhh kweli kwa shetan kunalipa
Wcb wanapenda kujipaisha tu amn lolote
👆👆👆👆👆👆👆😭😭😭😭
dah