Jose Chameleone aamua kupita nyayo za Bobi Wine ‘Watu wana kiu ya uongozi unaofaa na hawajaupata’
Msanii wa muziki wa Hip hop nchini Uganda Jose Chameleone hapo jana ameamua kufuata nyayo za Bobi Wine kwa kuingia kwenye siasa.
Inaelekea umekuwa ni mtindo wa kawaida kwa wanamuziki maarufu kugeuka kuwa wanasiasa. Bobi Wine amekuwa akizingirwa na utata wa kisiasa tangu alipogombea kiti cha ubunge mwaka 2017.
Kwa mujibu wa shirika la habari la BBC, Jose Chameleone ambaye jina lake halisi ni Joseph Mayanja amesema kuwa anataka kuwa Meya wa mji mkuu wa Uganda Kampala. Amenukuliwa na gazeti la Uganda Observer akieleza.
Chameleone ni mmoja wa wanamuziki maarufu katika eneo la Afrika Mashariki.
Moja ya nyimbo zake zinazofahamika ni ule wa Shida za Dunia, unaozungumzia matatizo yanayowakabili watu:
Thank you again @ComedyStoreUG pic.twitter.com/fLsO13Trwr
— JOSE CHAMELEONE (@JChameleone) April 5, 2019
Akielezea matarajio yake, amesema:”Wakati huduma zinapokuwa katika hali mbaya, watu wanaanza kuamka .Watu wana kiu ya uongozi unaofaa na hawajaupata”.
“Wale wanaodhani kuwa ni mkumbo wa Bobi Wine wana ukweli kiasi fulani ,” Chameleone alinukuliwa akisema.
Bobi Wine alipiga kengele halafu akasema ‘Tumekuwa watu wazima wa kutosha sasa ; Tunaweza kufanya hili ‘. Kwani kuna shida gani ya kufanya hilo? Kila kitu katika dunia hii kina mtu fulani aliyekianzisha .”
Chameleone anakiri kuwa ameshawishiwa na Bobi Wine. Muimbaji huyo wa kibao ”Badilisha” anaaminiwa kuwa amekuwa mfuasi wa chama tawala cha NRM, ambapo amekuwa akitumbuiza kwenye matukio ya chama hizo.
Chameleone hakuficha urafiki wake na mbunge wa Kyadondo mashariki Bobi Wine, hususan pale Wine alipojipata katika utata wa kisiasa na kukamatwa na maafisa wa polisi na kuwekwa mahabusu. Alimtembelea mahabusu kumfariji:
Today morning I woke up and went to Luzira Maximum prison to Visit my comrade, Bobi Wine, I was informed that I had to get clearance from the Commissioner General.
I tried to negotiate but it was all in Vain!… https://t.co/o6I4FMu0Gz
— JOSE CHAMELEONE (@JChameleone) April 30, 2019
Bwana Chameleone amekuwa akionyesha nia yake ya kuwa mwanasiasa kupitia jumbe zake za Tweeter.
#MAYANJA2021 | @JChameleone pic.twitter.com/UXcHylU1S1
— SENETA DAUDI WA KOTA (@DAUDIWAKOTA) April 13, 2019
We start another journey again #LordMayanja2021 🇺🇬 pic.twitter.com/tTBBAFsM5I
— JOSE CHAMELEONE (@JChameleone) April 15, 2019
On recent mission of patriotism we begun in Kawempe. Promised to further our message love, Patriotism through #BulungiBwansi Remarkable one we took spirit to Gaba Market,Later a friendly football match 100%Chameleone FC | Gaba Market FC.
Thanks for receiving us 🇺🇬 pic.twitter.com/MS0tVzJKbR
— JOSE CHAMELEONE (@JChameleone) May 4, 2019
Bobi Wine, ambaye Jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi, alichaguliwa kuwa mbunge alipogombea kiti hicho kama mgombea binafsi mwaka 2017.
Tangu kuchaguliwa kwake amekwishafanya maandamano maarufu na amekuwa akikamatwa na kushtakiwa kwa uhaini. Anadai kuwa alipigwa na polisi alipokuwa katika mahabusu ya polisi.