Habari

Kansela Angela Merkel ajiweka Karantini

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amejiweka Karantini baada ya kufahamishwa kuwa daktari aliyekutana naye siku ya Ijumaa, amegunduliwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Image result for German chancellor goes into self-quarantine

Msemaji wa Kansela Angela Merkel, Steffen Seibert ameyasema hayo hapo jana siku ya Jumapili.

Seibert ameongeza kuwa Kansela ataendelea kufanyiwa vipimo vya Virusi vya Corona kutokana na vya awali havijaonyesha. ”Merkel ataendelea kufanya kazi zake akiwa karantini yake,” amesema Seibert.

Hapo jana siku ya Jumapili, Merkel amesema kuwa taifa hilo linapitia wakati mgumu na hivyo kuwahasa watu kupunguza mawasiliano kadri inavyowezekana.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents