Habari
Kansela Angela Merkel ajiweka Karantini
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amejiweka Karantini baada ya kufahamishwa kuwa daktari aliyekutana naye siku ya Ijumaa, amegunduliwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.
Msemaji wa Kansela Angela Merkel, Steffen Seibert ameyasema hayo hapo jana siku ya Jumapili.
Seibert ameongeza kuwa Kansela ataendelea kufanyiwa vipimo vya Virusi vya Corona kutokana na vya awali havijaonyesha. ”Merkel ataendelea kufanya kazi zake akiwa karantini yake,” amesema Seibert.
Hapo jana siku ya Jumapili, Merkel amesema kuwa taifa hilo linapitia wakati mgumu na hivyo kuwahasa watu kupunguza mawasiliano kadri inavyowezekana.