Michezo

Kesi ya Aveva na Kaburu ngoma nzito

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema kuwa jalada la kesi ya utakatishaji fedha na kughushi inayomkabili Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ bado lipo kwa DPP.

Wakili wa Serikali, Vitalis Peter amemweleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa lakini jalada la kesi bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Aidha, amedai kuwa DPP ataangalia kama ameridhishwa na kesi hiyo ama ala, ambapo watasubiri kama uchunguzi umekamilika.

Baada ya kuelezwa hayo, Wakili wa utetezi, Evidius Mtawala kwa sababu ya taratibu zinazoendelea ni za kiofisi wanatumai jalada litaharakishwa.

Kutokana na hatua hiyo Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi October 4, 2017.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents