Habari

Kimbunga chasababisha maafa Cuba, watu 20 wadaiwa kufariki (Picha)

Kimbunga hicho ambacho kimeendelea kuimarika kinatarajiwa kuathiri miji ya pwani, na mpaka kufikia sasa watu 22 wameripotiwa kufariki katika visiwa vya Carebean.

Pia katika jimbo la Florida nchini Marekani watu milioni 5.6 ambao ni sawa na 25% ya watu wa maeneo hayo, wametakiwa kuhama makazi yao kujinusuru na kimbunga hicho kikubwa.

Kimbunga hicho kinakadiriwa kwenda spidi ya km 249 kwa saa, pia kimesababisha mvua kubwa na mafuriko, katika maeneo ambayo kimepita, huku kikisababisha watalii kukimbia nchi ya Cuba, na maelfu ya watu kukosa makazi.

Katika eneo la Berbuda takriban 95% ya majengo yake yameharibiwa hasara inayokadiriwa kufikia dola milioni 100.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents