Bongo Movie
Kuna watu wazima wamefyatuka, lazima tuwanyooshe – Hashim Kambi
Msanii mkongwe wa filamu, Mzee Hashim Kambi amesema amekua akiigiza katika maadhi ya filamu kama mzee kijana ambaye anapenda kula bata na mademu kwaajili ya kuwaelimisha watu wazima ambao akili zao hakiko sawa. Mzee huyo ameyasema hayo wiki hii akiwa mkoani Tanga katika uzinduzi wa ligi ya mpira ya wilaya ya Pangani ya Uweso Cup.