Burudani

Kundi la Bracket lakanusha uvumi uliosambaa Nigeria kuwa wao ni mashoga

Members wa kundi la Bracket ambao hivi karibuni wamemshirikisha staa wa Tanzania, Diamond Platnumz kwenye wimbo wao mpya, wamekanusha uvumi uliosambaa Nigeria kuwa wao ni mashoga.

bracket1

Kwa mujibu wa Naij.com, members wa kundi hilo Smash na Vast waliiambia SaturdayBeats kuwa mwanzoni baada ya kuzisikia taarifa hizo waliamua kukaa kimya kwa sababu ni za uongo.

“Sisi hatukutaka kuzungumzia suala hilo hadharani hapo kabla, lakini mimi nadhani inabidi tuzungumze. Tuliona hiyo habari na ilikuwa ya kuchekesha sana. Sisi hatukudhani kama itakuwa serious kiasi hicho mpaka mmoja wa wajomba zetu kutoka Enugu alipotupigia.”

Waliendelea,

“Hata wakati anatuuliza alikuwa akicheka. Mwisho wa siku, kuna baadhi ya mambo hutakiwi kusema hadharani lakini watu wanapaswa kusubiri mpaka wao waje kuona tukifunga ndoa. Hatuwezi kuanza kusema tuna girlfriends katika baadhi ya maeneo, au magirlfriends zetu ni kina nani. Lakini kwa kuweka mambo sawa, sisi si mashoga. Watu wanaotufahamu wanajua kwamba sisi si mashoga.”

Smash alimaliza kwa kusema:

“I am a proper Igbo man and there are certain things that my people expect from me before I can get married and once those things are cleared, I would look for someone to marry.”

Na Vast naye alisema ana girlfriend ambaye yupo Ethiopia:

“I have somebody and when I am ready, people would go with me to Ethiopia to get married.”

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents