Burudani

Lifahamu Elani: Kundi la Kenya linalotikisa kwa nyimbo zenye utunzi wa Kiswahili fasaha

Pamoja na kuanzishwa miaka kadhaa iliyopita, nimelifahamu kundi la Elani la Kenya kupitia wimbo wake uitwao Milele.

1604836_747098881980635_1698345294_n

Utunzi, uandishi na sauti za wimbo huo, vilinifanya niusikilize mara nyingi na kwa makini zaidi kwakuwa nilisikia kitu kipya kutoka Kenya ambacho kwa muda mrefu sijawahi kusikia.

1601468_745298508827339_51908482_n
Wambui Ngugi

10154342_750023888354801_2134140884_n
Maureen Kunga

Nilivutiwa na namna ambavyo utunzi wao umetumia Kiswahili fasaha kuliko nyimbo nyingi za Kenya ninazozifahamu. Kwa sifa hizo kwa sasa Elani kwangu ndio kundi bora zaidi Afrika Mashariki.

1966955_745833998773790_1442344715_n
Bryan Chweya

Siwezi kuacha kuusifia urembo wa wasichana wawili wanaounda kundi hilo, Wambui Ngugi na Maureen Kunga.

1795723_748957658461424_1659826804_n

Elani linaundwa na vijana watatu. Pamoja na Wambui na Maureen, yupo pia Bryan Chweya. Watatu hawa walikutana Alliance Française mwaka 2008 na haraka wakawa marafiki.

Haikuwa muda mrefu hadi walipogundua kuwa wote walikuwa wanapenda kufanya muziki na ndipo kundi la Elani likaanzishwa.

Elani ni neno la Giriama linalomaanisha mwanga. Wanasema wanataka kuwa mwanga wa dunia kupitia muziki wao.

1900150_734343303256193_87058519_n

Pamoja na muziki, Muthoni alisomea sheria kwenye chuo kikuu cha Nairobi, Wambui alisomea Actuarial Science kwenye chuo hicho pia na Bryan alisomea sheria.

December 6 kundi hilo liliachia album yake ya kwanza iitwayo “Barua ya Dunia” ikiwa na nyimbo kama Milele, Jana Usiku, Kuku, Barua, Zuzu, Peperuka na zingine.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents