BurudaniDiamond Platnumz

Mafikizolo: Collabo yetu na Diamond ni ‘moto wa kuotea mbali’

Kundi la muziki la nchini Afrika Kusini, Mafikizolo, limedai kuwa collabo yao na Diamond Platnumz ‘Colors of Africa’ ni moto wa kuotea mbali.

12353268_1255628367797209_1475659202_n

Member wa kundi hilo, Theo, amedai hadi sasa video yake haijatoka kwakuwa wamepanga kitu kikubwa zaidi kwaajili ya kuifanyia promotion.

12093403_1670903123153923_25252133_n

Theo alikuwa akimjibu shabiki aitwaye Frankestain Pastory, aliyemuuliza Instagram sababu za kuchelewa kwa video hiyo.

index

“Tunafahamu kuwa mashabiki wetu wanasubiri lakini tuna mpango mkubwa wa kimasoko kwaajili ya uzinduzi wa video,” alisema Theo.

“Mafikizolo na Diamond ni wanamuziki wakubwa sana Afrika hivyo uzinduzi wa wimbo na video yake unatakiwa kupangwa vyema. Ninachoweza kukuahidi ni kuwa video na wimbo vimesimama. Hatutowasubirisha kwa muda mrefu sana. Tafadhali kaka yangu kuwa mvumilivu, subira yako haitopotea bure.”

12353414_945724892143162_1179554654_n

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents