Michezo
Mahakama yapokea kesi ya kupinga uchaguzi TFF
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imepokea kesi ya kupinga uchaguzi wa Shirikisho wa Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na imemtaka Rais wake Wallace Karia, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi na Bodi ya Wadhamini ya Shirikisho hilo kufika Mahakamani kujibu hoja za kwanini uchaguzi wa TFF usimamishwe, wito huu ni wa kesho Ijumaa saa 3 asubuhi.