Majizzo ajibu mapigo kwa Diamond, anaziba njia ila yeye anapita tu
KLupitia kipindi cha RECAP NA MANDO @el_mando_tz amefafanua kwa urefu video aliyopost Majizzo baada ya kuamua kuhamishia Masanja kwenye joto la asubuhi kusoma magazeti.
Video imeeleza kila kitu kinachoendelea kati ya hao wawili wakurugezi wa moja ya media kubwa Tanzania, Majizzo amejigamba namna anavyovumbua vipaji kutoka kila kona ya nchini akitumia neno #Telescope
Diamond ameonyesha jeuri ya pesa kwamba atakachotaka kufanya atafanya kama kitahitaji pesa na hata kauli yake ya jana kuwa mafanikio chaya kwenye kampuni yanaletwa na uwekezaji na ubunifu.
Majizzo amemtumia mtu aliyevaa kanzu mithili ya Sheikh Mansour akionekana akimzibia njia lakini Majizzo anatabasamu na kutafuta njia nyingine ya kupita.
Kwa wakati mmoja vitu vyote vimethihirishwa na hawa wakurugenzi UBUNNIFU na UWEKEZAJI, haviachani