Burudani
Matonya na Tunda Man hawako sawa licha ya kudaiwa kumaliza tofauti zao
Matonya amesema hajawahi kuonana na hana shida ya kumtafuta rafiki wake wa zamani, Tunda Man.
Matonya na Tunda Man waliingia kwenye mgogoro baada ya Tunda kudai alikuwa anamwandikia nyimbo Matonya katika kipindi cha nyuma hali iliyoleta tofauti baina yao mpaka sasa.
Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio Jumatatu hii, Matonya alisema hajawahi kuonana na kuzungumza na Tunda Man siku za hivi karibuni.
“Hata kuonana naye sijaonana naye, hawa story zao achana nazo,” alisema. “Sijawahi kuzungumza hili suala na wala sina hiyo plan kabisa, yaani sijawahi kukaa na Tunda Man kumzungumzia hili suala.”