Habari
Mtengeni Trump – Obama awaasa viongozi wa juu wa chama cha Republican
Rais wa Marekani, Barack Obama amewaasa viongozi wa juu wa chama cha Republican, wajiondoe kumuunga mkono Donald Trump kama mgombea urais wa chama chao.
Kwenye mkutano wa kumpigia kampeni mgombea wa chama cha Democratic, Hillary Clinton, Obama alisema haina maana viongozi hao kupinga kauli za Trump wakati bado wakiendelea kumuunga mkono katika harakati zake za kuingia White House.
Viongozi wengi wa juu wa Republican wamejitenga na Trump baada ya kuvuja kwa video ambayo anasikika akiwadhalilisha wanawake. Alilazimika kuomba radhi.
Obama amesema maneno ya Trump dhidi ya wanawake, yanamnyima hata sifa za kuuza duka.