Bizzare

Mwanaume aliyeshauriwa na ‘Sangoma’ kufanya mapenzi na Punda atupwa jela

Mwanamme mmoja nchini Afrika Kusini aliyetambulika kwa jina la Ntando Mankungwini ametupwa jela mwaka mmoja baada ya kukutwa akifanya mapenzi na Punda.

Ntando (23) alikutwa usiku wa Jumatano ya septemba 20 mwaka huu kwenye zizi la nyumba jirani na nyumbani kwao mjini Mount Fletcher, Afrika Kusini akiwa nyuma ya punda usiku wa manane, kitendo ambacho wamiliki wa punda huyo walijua kuwa ni mwizi ila walikuja kustuka baada ya kumlika tochi na kumkuta akiwa utupu.

Wamiliki hao wa punda walimkamata na kumpeleka polisi na ndipo mtuhumiwa alikutwa na makosa ya unyanyasaji wa wanyama.

Mtuhumiwa akiwa Mahakamani alikiri kosa hilo la kufanya mapenzi na punda huyo huku akieleza kuwa alitekeleza sharti alilopewa na mganga wa kienyeji.

Ntando amesema alienda kwa Mganga wa Kienyeji kusaka dawa ya kuongeza nguvu za kiume na ukakamavu, ndipo aliposhauriwa kutembea na Punda.

Tayari mahakama ya mwanzo wilayani Mount Fletcher, Cape Town imetoa hukumu jana kwa kumfunga mwaka mmoja jela kwa kosa la unyanyasaji wa wanyama.

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents