Michezo

Nawahakikishia Disemba 11 tutawapiga – Tamko la Mwenyekiti wa Simba SC

Kupitia Mkutano Mkuu wa Mabingwa wa Nchi Simba SC Menyekiti mpya wa Bodi ya timu hiyo, Salim Abdallah Muhene “Try Again” amewaahidi mashabiki na wapenzi wa miamba hiyo ya soka kuwa Disemba 11 mtani wao Yanga atakufa pale kwa Mkapa kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara.

“Nawahakikishia Disemba 11 tutawapiga. Mbinu zote tunazijua. Tunachowaomba mashabiki ni umoja na ushirikiano.”- Mwenyekiti wa Bodi, Salim Abdallah Muhene “Try Again”.

Timu ya Simba SC mpaka sasa inashika nafasi ya pili kwa kuwa na pointi 14 huku wanaoongoza ligi Yanga SC wakiwa na alama zao 16 wakiwa na tofauti ya alama mbili (2) pekee mkapa sasa huku ligi kuu ikiwa bado mbichi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents