Habari

Nyoka amuua bosi wake

Maafisa wa Maryland wamesema bwana mmoja amekutwa amekufa nyumbani, kwake Kaunti ya Charles ambae anafuga nyoka zaidi 100 akiwemo aina ya vifutu na koboko.

Wachunguzi wameviambia vyombo vya habari kifo cha bwana huyo mwenye umri wa miaka 49 kimetokana na kung’atwa na nyoka kwa bahati mbaya.

Mamlaka ya eneo hilo inasema mwili wake ulikutwa huku kukiwa na nyoka 124 nyumbani kwake wakiwemo wenye sumu kali na kusababisha zoezi la kuuokoa mwili wake kuchukua masaa kadhaa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents