Michezo

Ofisi za TFF za fungwa na TRA

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imezifungia ofisi za shirikisho la soka Tanzania (TFF).

TRA kupitia Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart imewataka wafanyazi kuacha kila kitu cha shirikisho hilo ndani.

Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amethibitisha hilo na kusema TFF haikutimiza walichokubaliana kuhusiana na wanachowadai. alipo ongea na chombo kimoja cha habari

“Ni kweli tumezifunga na hiyo ni hatua ya mwisho kwetu kufanya hivyo. Tulikubaliana kulipa tunachowadai na muda umepita,” alisema.

Alipouliuzwa kuhusiana na kiasi: “Haya ni masuala ya sisi na wenyewe.”

Yono ndio waliohusika katika kuzifunga ofisi hizo na kuwataka wafanyakazi wote kutotoka nje ya ofisi na kuacha kilakitu ndani.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents