Picha: Bondia Phil Williams wa Marekani atua Dar kumkabili Francis Cheka Ijumaa hii
Bondia wa Marekani Phil Williams ametua nchini kwaajili pambano lake la raundi 12 dhidi ya Francis Cheka/ Pambano hilo litafanyika Ijumaa ya August 30 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Mdau wa michezo nchini Said Kindeka kushoto akiwa na bondia Phil Williams wa Marekani
Pambano hilo ni la kuwania mkanda wa WBF na kumpata bingwa mpya wa Super Middleweight.
Francis Cheka, ambaye kwa sasa ni bingwa wa IBF Continental Africa anarekodi ya kushinda mapambano 28, 16 ni KO na kushindwa mara saba tu.
Phil “The Drill” Williams, anayetokea Minneapolis, Minnesota, Marekani ana rekodi ya kushinda mapambano 12, 11 KOs na kushindwa mara 5.
Bondia Phil Williams
Phil Williams akiwa na mkanda wake wa ubingwa
Phil Williams akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mchezo huo
Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ kulia akiwa na Phil Williams baada ya kutua nchini
Picha: www.superdboxingcoach.blogspot.com