Habari
Picha: Kesi ya Halima Mdee yapigwa tena kalenda
Kesi ya kutoa lugha chafu inayo mkabili Mbunge wa Kawe,Halima Mdee imeahirishwa mpaka September 12 mwaka huu, kutokana na upelelezi kutokamilika.
Halima mdee anatuhumiwa kutoa lugha Chafu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli katika mkutano wake katika Baraza la Wanawake Chadema(BAVICHA).
Mawakili wa Halima Mdee, wakiongozwa na Wakili Hekima Mwesigwa wamewasilisha pingamizi hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa. Ambapo kesi hiyo imeahirishwa mpaka tarehe tajwa hapo juu.
Hata hivyo Halima Mdee, alikamatwa Julai 4 2017 na Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Kinondoni Dar es salaam kwa agizo la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi.
Picha: Salum Kaorata
Na Emmy Mwaipopo