Picha: Mamia kwa maelfu wajitokeza kuupokea mwili wa Albert Mangwea, vijana wasikika wakiimba kulitaja jina lake
Mamia ya wakazi wa Dar es Salaam wakiwemo wasanii wa muziki na filamu nchini leo wamejitokeza kuupokea mwili wa marehemu Albert Mangwea kwenye uwanja wa ndege wa Mwl Julius Nyerere uliowasili kutoka nchini Afrika Kusini.
Wasanii Dollo na KR Mulla
Bongo5 imeshuhudia umati mkubwa wa mashabiki wa Mangwea aliyefariki wiki iliyopita nchini humo uliokuwa na hamu kubwa ya kushuhudia jeneza lililokuwa na mwili wake.
Baadhi ya vijana waliokuwa wakiiimba kwa sauti waliizingira gari iliyokuwa na mwili na kutaka walibebe jeneza kwa mkono na hivyo kuufanya msafara uliokuwa ukielekea kwenye hospitali ya Muhimbili usimame kwa muda bila kusogea.
Umati wa watu ukisubiri kuona gari lililobeba mwili wa Mangwea
Vijana wakiimba nyimbo za kuomboleza
Vijana hao ambao wengine walionekana wakilia kwa uchungu wamesikika wakiimba ‘Tumshushe, Tumbebe’.
Hali hiyo imepelekea kuzuka kwa vurugu iliyowapa wakati mgumu polisi waliosambazwa kuangalia hali ya usalama.
Wasanii mbalimbali wameonekana wakipokezana kubeba msalaba kuliongoza gari lililobeba mwili baada ya wananchi kuwataka washuke kwenye magari.
Mtangazaji wa Times FM, JABIR SALEH Ametweet: P funk ameamua kukimbia na kutembea na wana ili folen iende!!!much lov kwa p anakimbia hadi anatia huruma!”
Umati mkubwa kwenye uwanja wa ndege
Mkoloni na Profesa Ludigo
Fid Q alikuwa mmoja ya wasanii waliojitokeza
Hafsa Kazinja na Quick Rocka wakiwa na simanzi
Chege
Abdul Kiba, Hafsa Kazinja na Sauda Mwilima
Izzo B akiwe mwenye majonzi makubwa
Mrisho Mpoto
Young Killa
Mwili wa Mangwea ukiwa umebebwa
Shabiki wa Mangwea akilia kwa uchungu
Ni majonzi tu
Dr Cheni
Picha zaidi zinafuata.