Burudani
Picha: Peter wa P Square alivyo kutana na wachezaji wa Chelsea
Mwanamuzi wa kundi la P Square kutoka Nigeria, Peter ni shabiki mkubwa wa club ya Chelsea kipindi cha nyuma aliwahi kuwa kwenye academy moja na John Mikel Obi miaka 20 iliyopita wakiwa na ndoto za kucheza soka siku moja.
Peter wikiend hii alisafiri hadi England kwenda kuangalia mechi ya Chelsea Vs United , Baada ya mechi alitumia muda wake kupiga picha na kukutana na mastaa mbalimbali wa Chelsea.
Kuna taarifa kwamba Peter anataka kufungua kampuni kwa ajili ya kusimamia wachezaji soka. Peter ame-tease habari hiyo kwa kutumia hashtags za kwenye post yake ambapo ameitaja kampuni hiyo kwa jina na P Classic Football Management (PCFM)