Picha: Vilio na simanzi vya tawala kuaga miili ya wanafunzi 32 Arusha
Ni vilio na simanzi zimetawala katika kuaga miili ya wanafunzi 32, walimu 2 pamoja na dereva mmoja waliopoteza maisha kwa ajili ya gari Jumamosi hii huko mkoani Arusha.
Wananchi wakiwa amejitokeza kwa wingi katika uwanja wa Sheikh Abeid Karume Arusha kuaga miili ya wanafunzi 32, walimu 2 na dereva mmoja.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan yuko mjini Arusha muda huu ambapo anaongoza wananchi wa mkoa huo pamoja na mikoa ya jirani katika kuuaga miili ya wanafunzi 32, walimu Wawili pamoja na dereva Mmoja wa shule ya Lucky Vincent iliyopo mkoani humo.
Wanafunzi na walimu hao walipata ajali hiyo wakati wanaenda kwenye shule iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mitihani wa ujirani mwema baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kutumbukia korongoni kwenye eneo la Rhotia wilayani Karatu.