Habari
Picha: Wasichana waliokuwa wametekwa na Boko Haram wakutana na familia zao
Baadhi ya wasichana takriban 250 wa Nigeria waliokuwa wametekwa na wapiganaji wa kundi la Boko Haram, April mwaka 2014, wameachiwa huru.
Alhamis ya October 13, serikali ya Nigeria ilitoa taarifa za kuachiwa kwa baadhi ya wasichana hao na kurejeshwa nyumbani baada ya mazungumzo kati ya viongozi wa serikali na Boko Haram.
October 17, wasichana 21 wa Chibok walikutana na familia zao kwa mara ya kwanza baada ya miaka kibao. Hizi ni baadhi ya picha.