Habari
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Jumatano hii alimteua Doto M. James kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.
Kabla ya uteuzi huo James alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera).
Doto M. James ameapishwa leo Septemba 1, 2016 saa 2:45 Asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Kufuatia uteuzi huo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile atapangiwa kazi nyingine.
Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa
BY: EMMY MWAIPOPO