Habari
Rais Obama kukutana na Trump White House
Rais Barack Obama, anatarajia kuwa mwenyeji wa rais mteule, Donald Trump kwenye ikulu ya White House kwa mazungumzo yanayoweza kurahisisha ukabidhianaji wa madaraka.
Huo unaweza kuwa mkutano mgumu kwakuwa Trump amewahi kuhoji uraia wa Obama wa Marekani na kuahidi kufuta baadhi ya sera zake muhimu. Obama hata hivyo amesema yuko nyuma ya Trump baada ya kushindwa vibaya kwa Hillary Clinton.
Wakati huo huo maelfu ya raia wa Marekani wameingia mtaani kupinga kuchaguliwa kuwa rais kwa bilionea huyo.