Crazy GK awahimiza wasanii kuitangaza Tanzania kwenye video zao
Rapper King Crazy GK amesema ni busara kwa wasanii wa Bongo Flava kutangaza vivutio vilivyopo Tanzania katika video zao badala ya kutangaza mazingira na vivutio vya mataifa mengine.
Kupitia kipindi cha The Splash kinachosikika kupitia Ebony FM, GK amesikika akisema kuwa, “Tanzania kuna vitu vingi sana vya kustaajabisha,ambavyo mara chache unaweza kuvipata nje kuna Mlima Kilimanjaro kuna vitu vya akina Mkwawa kuna vitu vingi ambavyo ukivionyesha dunia ina wonder.”
GK ameongeza, “Mzuri pesa umeiona nilimchukua Director wenye exposure nikashoot katika location ambazo wanazitumia wanamuziki wa kawaida hapa Tanzania lakini nilivyozitumia kila Mtanzania ameshangaa. Tuitambulishe zaidi Tanzania kimataifa tayari wenzetu South Africa wameshajitangaza tunaongezea kuwatangaza.”
https://www.youtube.com/watch?v=4mWcHk6kPzQ
Hivi karibuni GK aliachia wimbo wake uitwao Mzuri.
BY CHRIS BEE