Habari
Ray J aja na remix ya ‘I Hit it First’ iliyowataja wazi kwa majina Kim K na Kanye West
Baada ya kuzungumziwa sana katika vyombo vya habari wiki kadhaa zilizopita kutokana na wimbo wake mpya ‘I hit It First’ wenye sababu za kutosha kuamini kuwa ni diss ya Kim Kardashian na Kanye West, Ray J amekuja na remix ya wimbo huo.
Katika remix hiyo kaka huyo wa staa wa kike Brandy amewashirikisha Dorrough, Uncle Murda, Clyde Carson na wengine.
Kile kinachoonekana kuwa ‘Kama mbwaimbwai’ katika remix hiyo Uncle Murda anaanza verse ya kwanza kwa maneno “Everybody know this record about Kim K. The video girl look like Kim K. Waiting to hear a response from Kanye…”
Isikilize hapa