Michezo
Ronaldo apewa mtihani mwepesi na Real Madrid kama kweli anataka kutua Juventus
Klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania imemtaka nyota wake, Cristiano Ronaldo kuwaeleza mashabiki kuwa halazimishwi kuondoka ndani ya timu hiyo na kutua Juventus.
Rais wa Real, Florentino Perez na Mkurugenzi wake Jose Angel Sanchez wanahofia mashabiki kutoa lawama zao za kumruhusu Ronaldo kutua Juve kwa dau la euri milioni 100 ikiwa sawa na pauni milioni 88.
Wakala wa Ronaldo, Jorge Mendes (kushoto) akiwa na Ronaldo
Wakala wa Ronaldo, Jorge Mendes amesema kuwa mchezaji wake akifanikiwa kuondoka ndani ya klabu hiyo basi itabaki kuwa ndani ya moyo wake, rais wake, uongozi bila kusahau mashabiki wa Real Madrid duniani kote.