Habari
Sababu za Mama Janeth Magufuli kuguswa kutoa msaada wa chakula kwa wafungwa hizi hapa (+video)
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Janeth Magufuli amewataka Watanzania kuondoa dhana potofu ya kuamini waliopo gerezani ni wahalifu bali hata wao wanahitaji msaada na faraja wakiwa huko.
Ameyasema hayo leo wakati akikabidhi chakula kwa wafungwa wa Gereza la Ukonga ambapo ameeleza kuwa wapo wagonjwa, wazee, watoto na wasiojiweza hali iliyopelekea kuguswa kuwapelekea msaada.