HabariSiasa

Shuhudia namna kiongozi wa Upinzani Korea alivyochomwa kisu ubavuni na shingoni

Kiongozi wa upinzani nchini Korea Kusini alichomwa kisu katika mkutano na waandishi wa habari katika mji wa Busan, shirika la habari Yonhap limeripoti.

Lee Jae-myung, ambaye alikosa nafasi ya urais wakati wa uchaguzi mkuu wa urais mwaka 2022, alichomwa kisu upande wa kushoto wa shingo yake majira ya asubuhi Jumanne.

Mshambuliaji alikamatwa katika eneo la tukio.

Bwana Lee alipelekwa hospitali mara tu aliposhambuliwa. Alikuwa katika hali mbaya wakati huo, Yonhap imesema.

Aliyefanya mashambulizi alikuwa ana kati ya miaka 50 au 60, taarifa zilieleza.Aliripotiwa kuwa alikuwa amemkaribia bwana Lee ili kumuomba saini yake, kabla ya kumchoma kisu.

Picha za Video zinazoonesha shambulio hilo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonesha bwana Lee akianguka katikati ya mkusanyiko wa watu, wakati baadhi ya watu wakijaribu kumkamata mshambuliaji.

Picha zinaonesha tukio hilo la bwana Lee lying akiwa amelala chini huku amefumba macho huku mtu mmoja akiwa amemuwekea kitambaa katika shingo.

Bwana Lee, 59, anayeongoza chama cha Democratic Party of Korea ambaye kwa sasa sio mbunge lakini anatarajiwa kuwania uongozi katika uchaguzi ujao unaotarajia kufanyika mwezi Aprili 2024.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents