Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara Simba SC hii leo hawakuzungumza na waandishi wa habari katika Mkutano uliyofanyika Makao Makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF licha ya Kaimu Afisa Habari wa timu hiyo kufika mahala hapo.
Baada ya kuzungumza Kocha Nabi wa Yanga, ulifika muda wa Simba nao kuzungumza kwenye Mkutano huo uliyokuwa ukirushwa Live na baadhi ya vyombo vya habari, lakini Chiko ambaye ni Kaimu Afisa Habari wa Simba hakuzungumza bali alionekana kama kupishana maneno na baadhi ya aliyeongozana naye.