Michezo

Suala la maslahi linavyoendelea kulitafuna soka letu la Afrika, timu ya Uganda yaelezwa kususia mazoezi nchini Misri kisa maslahi

Suala la maslahi linavyoendelea kulitafuna soka letu la Afrika, timu ya Uganda yaelezwa kususia mazoezi nchini Misri kisa maslahi

Wachezaji wa Uganda walisusia mazoezi Jumanne katika mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika kwasbababu ya mzozo wa malipo, kwa mujibu wa shirikisho la soka nchini humo (FUFA). Ni mzozo wa hivi karibuni kutokea katika mashindnao hayo kufuatia hali kama hiyo kujiri kwa wachezaji wa timu za Zimbabwe, Nigeria na Cameroon.

Kwa mujibu wa BBC. Timu hiyo ya Cranes iliibuka nafasi ya pili katika kundi lake na inajitayarisha kukabiliana na Senegal katika timu 16 bora Ijumaa.

FUFA linasema wachezaji hao wanajaribu kujadili upya masikizano katika mkataba uliosainiwa kati yao.

Linasema kuwa makubaliano yalifikiwa kabla ya mahsindnao na limetaja malipo ambayo tayari yametolewa kwa wachezaji hao.

“Kufikia tarehe 2 Julai 2019, kila mchezaji alikuwa amepokea hadi $14,600 … na marupurupu ya ziada ya kila siku na kitita cha ushindi kinachowasubiri,” taarifa hiyo imesema.

“Tunatarajia wachezaji watabadili uamuzi wao na warudi uwanjani Jumatano,” msemaji wa FUFA ameiambia BBC.

wachezaji hao hawajatoa kauli kufikia sasa.

Nigeria, Zimbabwe na Cameroon pia zimekabiliwa na hali hiyo katika kuelekea kwa mahsindano hayo nchini Misri 2019 au tangu mashindano hayoyaanze.

Visa vyote hivyo vilitatuliwa pasi kutatuza mashindano hayo.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents