Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruguay, Luis Suarez amesema kuwa kamwe hawezi kuomba radhi kwa Ghana kutokana na kitendo chake cha kufunga goli kwa mkono katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010.
Suarez amesema angeomba radhi kama tu, angemjeruhi mchezaji lakini Ghana wenyewe walipata mkwaju wa penati na mchezaji wao akakosa.
Nakuongeza kuwa alisherehekea kitendo cha Ghana kukosa penati kama vile wamefunga goli.
Nyota huyo amesema hayo wakati timu yake ya Uruguay ikijiandaa kukabiliana tena na Ghana hapo kesho kwenye michuano hiyo ya Kombe la Dunia nchini Qatar.