Burudani

Surprise: Huddah na Annabel wa Kenya waelekea Afrika Kusini katika fainali ya ‘The Chase’, baada ya kusema hatahudhuria! (Picha)

Siku mbili zilizopita Huddah Monroe alitweet kusema kuwa hataweza kuhudhuria fainali za Big Brother ‘The Chase’ itakayofanyika Jumapili hii nchini Afrika Kusini kutokana na sababu zisizozuilika.

monroe

Taarifa hiyo ilionekana kuwasikitisha mashabiki wake wengi ambao walikuwa na shauku ya kumuona mshiriki huyo wa Kenya kwa mara nyingine kupitia camera za DSTV kwa mara ya mwisho kwenye The Chase.

hudda2
HUddah na Annabel

Wote tukiwa tumeshaamini kuwa Boss Lady hatakuwepo katika fainali hizo, leo Huddah ametu-surprise kwa kupost picha akiwa na mshiriki mwenzake wa ‘The Chase’ Annabel na kuandika “With Annabel heading to SOUTH AFRICA…..JOBURG’ we comin baby…….large up urselves!”

Pia masaa matatu yaliyopita Annabel naye alitweet “Off to SA with my girl @HUDDAHMONROE woop! Woop!”.
Hii inamaanisha zile sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa Huddah kumsababisha kushindwa kwenda Afrika Kusini kama alivyokuwa amesema zimetatuliwa, au nashawishika kuamini kuwa tweet yake ya juzi ya kutohudhuria fainali hizo huenda alitaka kuona kiasi gani watu watasikitika kusikia habari hiyo!!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents