Bongo Movie
TAFF ladai halikubaliani na kushushwa kwa bei ya filamu
Shirikisho la filamu Tanzania, TAFF, limesema halikubaliana na uamuzi uliochukuliwa na kampuni ya Steps Entertainment kuhusu kushusha bei ya filamu kutoka shilingi 3,000 hadi 1,500.
Rais wa shirikisho la filamu, Simon Mwakifwamba
Mwakifwamba ameiambia Bongo5 kuwa wasanii wanafanya kazi kubwa na hivyo bei ya filamu haiwezi kushushwa kama inavyoshushwa kwenye bidhaa nyingine. “Sisi hatukubaliani na hilo suala, kuna vikao vilikuwa vikiendelea kuhusu hili suala na Jumanne wiki ijayo tutatoa kauli,” amesema.