Burudani
Tip Top kula Idd Dodoma
Kundi la muziki la Tip Top Connection, linatarajia kuwasha moto katika mkoa wa Dodoma katika siku ya sikuku ya Idd, baada ya kutoka kufanya show katika mkoa wa Mbeya. Kiongozi wa kundi hilo Madee amesema akirudi huko anakuja kumtambulisha Dogo mpya katika kundi
hilo, ambaye video yake imekamilika hivi karibuni.