Burudani
Tunda Man kuja na filamu fupi ya Mama Kijacho
Pamoja na video ya wimbo wake ‘Mama Kijacho’, Tundaman amesema ataachia filamu fupi yenye jina hilo.
Muimbaji huyo amesema filamu hiyo itakayokuwa ikielezea kisa cha Mama Kijacho itatoka baada ya video ya wimbo huo.
“Video tayari ila sasa hivi tupo kwenye mpango wa kushoot short film ya Mama Kijacho,” Tunda aliambia E-News ya East Africa Television Jumapili hii.
“Ndani ya filamu utawaona akina Riyama, mimi mwenyewe pamoja na wahusika wengine wengi. Nilishawahi kufanya filamu mara moja kwenye movie ya mtu ilikuwa hainihusu sana lakini hii inanihusu mimi kama mimi. Kwahiyo watu wasubirie kazi nzuri,” alisema.
Tunda amesema ameamua kumtumia Riyama na waigizaji wengine ili kuvutia na kuleta maana halisi ya wimbo huo.