Burudani

Vanessa Mdee ashirikishwa na Shaydee wa Nigeria, kushare jukwaa moja na 2Face na Iyanya Lagos Alhamis hii

Vanessa Mdee yupo nchini Nigeria anakoendelea na ziara kwenye vyombo mbalimbali jijini Lagos.

11428169_808190649297048_692167330_n
Vanessa Mdee akihojiwa kwenye studio za Trace Nigeria

Tayari ameshazunguka na kuhojiwa kwenye vituo vyote vikubwa vya redio na TV nchini humo kupromote single yake ‘Nobody But Me.’

Akiwa huko Vee Money ameshirikishwa kwenye wimbo wa msanii Shaydee utakaotoka hivi karibuni.

“Sexyyy record with a sexyass chocolate beauty! cant wait.. @vanessamdee x @shaydeeboi, #Tanzania #Nigeria,” ameandika msanii huyo kwenye kipande cha video alichokiweka kwenye mtandao wa Instagram.

10354494_1618264841792405_2003753600_n
Vanessa akiwa studio na msanii wa Nigeria Shaydee aliyemshirikisha kwenye wimbo wake

Naye Vanessa amepost picha akiwa na msanii huyo na kuandika, “Shaydee On The Single x Money on The Track … I’m calling S.O.S @shaydeeboi you a bad man, the FIRE THOUGH!”

Katika hatua nyingine Alhamis hii Vanessa Mdee ataungana na 2 Face na Iyanya kwenye show iliyopewa jina 2 Face and Friends Grand Party.

11410722_1603684979890172_914205792_n

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents