Burudani
Nitaendelea kutoa nyimbo zenye ladha ya ‘Niroge’ na ‘Hawajui’ – Vanessa
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Vanessa Mdee, amefunguka kuwa nyimbo zake Niroge na Hawajui zote ameziweka katika mfumo mmoja.
Akiongea na kipindi cha Twenzetu cha Times FM, Vanessa alisema anataka kuubadilisha muziki wake na kuuweka katika mahadhi na ladha ya Kiswahili zaidi.
“Yeah Niroge na Hawajui ni idea moja, mfumo ni ule ule tu, yaani nataka nipite kwenye mfumo huo huo, so nilikubaliana na wenzangu tupite humu.”