Michezo
VIDEO: Kocha mpya wa Yanga awataja Simba, akumbushia walivyokutana Champions League
Klabu ya Yanga imemtangaza Kocha wake Mkuu Nasreddine Nabi kurithi mikoba ya Cedric Kaze, Mtunisia huyo aliwahi kuifundisha El Merreikh ya Sudan kabla ya kutimuliwa baada ya kutoka sare na Simba SC kwenye mchezo wa Klabu Bingwa kufuatia kutokuwa na matokeo mazuri kwenye michuano hiyo ya CAF.