Burudani

Wanataka kuufungia wimbo wangu mpya ‘Viva Roma viva’ kisa tu nimeongea ukweli – Roma

Saa chache baada ya wimbo mpya wa Roma ‘Viva Roma viva’ kutoka September 9, rapper huyo amedai kuwa ametishiwa wimbo huo kufungiwa.

roma new pic

Kupitia Instagram, majira ya saa mbili usiku Roma aliandika;

“WANATAKA KUIFUNGIA NYIMBO YANGU!! KISA TU NIMEONGEA UKWELI!! INANIUMA SANA NATAMANI HATA KULIA NIKIONA UKWELI HAUPEWI NAFASI!! NIOMBEENI NA MNIKUMBUKE KWENYE SALA ZENU NDUGU ZANGU!! Viva Roma viva”

ro

Bado haijafahamika sababu ya wimbo huo kutaka kufungiwa, na Roma hakupatikana kwenye simu yake nilipomtafuta kwaajili ya kuzungumza nae kuhusu swala hilo.

Usikilize hapa kama bado hujausikiliza

Hizi ni baadhi ya comments za mashabiki wake waliotoa maoni yao kwenye post hiyo;

paul2297:
Siku zote ukweli haupendwi na walanguzi na wezi kama ccm, na ninakupongez sana we ni miongoni mwa wasanii wanaojielew, hata kama wakilifungia leo tunashukuru mungu hataa ndege wa angani wameshalidaka nyimbo yako na wataendelea kuimba ukweli daima

stella_njau:
Usjal kaka tutakuombea watu kama nyiny tunawahtaji sana katika kuleta ukomboz najua its not easy kwako coz nchi yetu ni kandamiz but God is dere to protect u from those damb, selfish and lust leaders VIVA ROMA VIVA FOREVER tuko pa1 bro

oscarhimxelf:
Mimi huwa najiuliza ivi ulichoimba wewe na alichoongea slaa au mambo ambayo wanayoongea viongozi kwenye majukwaa ya kampeni mbona hayana tofauti kwann wao huwa hawafungiwi.. mfano juzi slaa akawa anaongea mpaka habar za maaskofu sijui kupewa hela na data nyingine mbalimbali ambazo alisema sikuona ile hutuba imefungiwa bali adi leo inatumika kama kielelezo lkn ww ukiongea kwann waseme ifungiwe …

mikemrossotza:
Hata waufungie kaka mkubwa mzigo tunao wamechelewa
seniorita_tynaalex Roma we ninoma nimeipenda nyimbo yako I salute you dear mpambanaji mwenzangu

galla_bway:
Kila wanachofanya wanachelewa broo ..ucwaze tutasambaza kuhakikisha jamii unaisikia huu wimbo …pamoja

levi_mkushflani:
HAHAHAHA WANAIFUNGIA WAKAT YLTUSHAIDOWNLOAD!? cc tunayo na ujumbe tushaupata

rosewau:
Mi nilijua tu…lazima ifungiwe…so jiandae tu wangu…

shabani_maulidi:
Viva #Roma#viva ukweli unauma wakifungia tutasikiliza hata kwenye simu bodaboda Bajaj daladala na majumbani kwetu message sent #viva#Roma#viva

eetaamajiko:
Usijal @roma2030 kitaa tushaipata na ujumbe umetufikia, hii inanikumbusha wimbo wa @nashMc kaka suma walifungia ukwel uliowazi kama vazi la kahaba,Wenyewe kwenye kampeni zao wanatukana ila hawafungiwi

francy_0903:
Sheria zingine zinavyopitishwa kwa kwel wanabid wàngalie kwa umakin kama mtu akisema ukwel anfungiwa maana matus ndo yamekatazwa sasa hata ukwel hawautaki loh tunapoelekea ni pabaya kwa kwel maana hamna wa kutuongelea juu ya nchi yetu zaid ya sisi wenyewe hawez toka mtu Marekan aje aongee ukwel juu ya Taifa letu coz hana uchungu kama sie wenyewe tuliomo ndan ya Taifa,hongera roma wimbo mzur and u r in my prayers

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents