Wasanii watatu wa label ya The Industry wapo tayari kuingia vitani
Mkurugenzi wa label ya The Industry, Nahreel amefunguka kwa kusema kuwa maandalizi ya kuwaleta wasanii wa label hiyo yapo katika hatua za mwisho.
Mmoja kati ya wasanii wa label ya The Industry, Rose
Akiongea na Bongo5 Jumamosi hii, Nahreel amesema tayari wasanii hao watatu kila mmoja ana video yake mkononi ambayo imeandaliwa Afrika Kusini na director Justin Campos.
“Hivi sasa kila msanii anakaribia kukamilisha albamu yake, na tuna video ambazo zipo tayari za wasanii wote watatu na video zimeandaliwa Afrika Kusini na Justin Campos, kwa hiyo sasa hivi tunaangalia jinsi ya kuanza kurelease moja baada ya nyingine,” alisema Nahreel.
Kwa upande wa Kundi la Navy Kenzo, Nahreel amesema wanajipanga kuja kivingine huku akiweka wazi ujio wa kobalo yao na mkali wa Aje, AliKiba.