Bongo5 ExclusivesBurudaniHabari
Wema Sepetu: Nilikutana na Whozu akiwa sinngle, sikuharibu mahusiano yake na Tunda
Mwanamitindo na msanii wa Bongo Movie @wemasepetu amefafanua kwa urefu zaidi namna mahusiano yake na @whozu_ yalivyoanza.
@wemasepetu ameeleza kuwa wakati anakutana na @whozu_ na kuanza kumtongoza kipindi kile @whozu_ hakuwa kwenye mahusiano yoyote.
Pia ameongeza kuwa @whozu_ baada ya kumtongoza ilichukua takribani miaka miwili hadi kumkubalia.
Jana kwenye Iftar yake Tz Sweetheart @wemasepetu aliulizwa na @el_mando_tz kuhusu ukaribu wake na mastaa mbalimbali maana wengi hawakuhudhuria kwenye Iftar yake.
Lakini pia aliulizwa kuhusu yale maneno ya mtandaoni kuwa ana ugomvi na @hamisamobetto
@wemasepetu ameweka wazi kabisa kuwa hana ugomvi wowote na @hamisamobetto na ndio maana hata kwenye Iftar yake alimualika.