Michezo
Yanga yazua gumzo

Baada ya Simba Sc kupoteza dhidi ya Prisons (1-2) na kushinda (1-2) dhidi ya Coastal Union, imeibua moja ya hoja ‘DHAIFU’ kwa baadhi ya Mashabiki maarufu na baadhi ya wachambuzi kwenye media mbalimbali.
Madai makubwa ni kuwa udhamini wa kampuni ya HAIER inayodhamini Klabu ya
, Namungo, Coastal Union inasaidia Yanga kushinda michezo yake kwa kile wanachodai kuwa kuna (CONFLICT OF INTEREST) uwezekano wa kupanga matokeo na kuzipa motisha timu zinazocheza na Simba SC.
Kitu kinacholeta mtafaruku ni baadhi ya wachambuzi wanaaminisha watu kuwa kinachosemwa ndio cha ukweli. Tukienda kwa Hoja. Kanuni na Sheria za (FIFA) na (CAF) hazikatazi kampuni moja kudhamini vilabu tofauti katika Ligi moja.
FIFA inazuia vilabu zaidi ya kimoja kumilikiwa na kampuni au mtu mmoja ndani ya Ligi moja, na wala sio kuzuia Udhamini (SPONSORSHIP). Hili swala la kampuni moja kudhamini timu tofauti katika ligi moja halijaanza leo Tanzania iwaje hoja zinaibuka sasa?
Kabla ya @moodewji kuwa na hisa 49% Simba alikuwa mmiliki wa klabu ya Africa Lyon, wakati huo akiwa mfadhili wa klabu ya Singida United hoja hizi za sasa wala hazikuibuka muda huo iwaje sasa? Bakhresa kupitia Azam anadhamini vilabu vyote vya ligi kuu na ana timu ya Azam hapo je?
@DStv wanadhamini klabu zote za ligi kuu ya South Africa lakini pia wana timu kwenye ligi hiyo iitwayo Supersport hawa nao hawana fair competition? Vipi kuhusu Vunjabei, Binslum na Sportpesa kudhamini timu zaidi ya 1 kwenye Ligi kuu?
@SimbaSCTanzania– Vunjabei. Prison – Vunjabei. Polisi Tanzania – Vunjabei. Singida Fountain Gate – Vunjabei. Coastal Union – Binslum Tyres. Stand United – Binslum Tyres. Mbeya City – Binslum Tyres. Ndanda – Binslum Vee Rubber. Simba – Sportpesa. Yanga – Sportpesa.

Singida FG – Sportpesa. Namungo – Sportpesa. Yanga msimu huu mpaka sasa ameshinda mechi 15 kati ya 17, katika michezo aliyoshinda ni timu mbili tu zinazodhaminiwa na HAIER, Kwani HAIER anaidhamini klabu yoyote huko (CAF),
wanawezaje kufika fainali (CAFCC)?
@YoungAfricansSC wanawezaje kufika Robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika (CAFCL) tena kwa kumpiga vibaya Bingwa wa Algeria mara nne mfululizo CR Belouizdad?. Ifike hatua tukubali ubora wa timu ya Yanga SC.
Tukiangalia Ligi kuu ya Afrika Kusini
@KaizerChiefs pamoja na @orlandopirates wote wanadhaminiwa na mdhamini mmoja ambaye ni kampuni ya Vodacom. Je nako hakuna Conflict of Interest? tukubaliane na ubora wa Yanga kwa sasa.
Credit kutoka kwa @zechicharito1
Imeandikwa na Mbanga B.