Michezo
Chuji apata shavu Ndanda FC
Kiungo wazamani wa Yanga SC, Athumani Iddi ‘Chuji’ amesaini kandarasi ya mwaka mmoja ya kuitumikia klabu ya Ndanda FC inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara.
Chuji sasa ataitumikia Ndanda FC ya mkoani Mtwara ambayo imeonekana kusuasua msimu uliopita.
Mwaka 2009 ambapo kiwango cha mchezaji huyo kilipo onekana kushuka aliingia katika matatizo na kocha Maximo katika timu ya taifa na klabu yake, Dusan Kondic, lakini bado walikuwa wakisema kuwa hakuna kiungo kama Chuji katika nyakati za sasa nchini.
Juhudi kubwa zimefanywa na Chuji katika kuhakikisha anarejea katika Ligi Kuu ya Vodacom na siku za hivi karibuni ameoneka kufanya vizuri zaidi katika michuano ya Ndondo FC.
By Hamza Fumo