Burudani
Familia ya Kardashian yamtaka Khloe ampige chini boyfriend wake French Montana
Familia ya kina Kim Kardashian hairidhishwi na ndugu yao Khloe kuendelea kuwa na French Montana hivyo inadaiwa kumshinikiza ampige chini.
Kwa mujibu wa TMZ, Chanzo cha karibu na familia hiyo kimedai kuwa familia ya Kardashian imemshauri Khloe aachane na Montana kwasababu wanaamini sio mwaminifu na anamsaliti ndugu yao.
Wanadai kuwa hivi karibuni wakiwa Dubai French alionekana na mwanamke mwingine mrembo, huku akimtumia dada yake Khloe, Kim Kardashian kufunika uovu wake.
Inadaiwa kuwa dalili za kusalitiwa zilikuja baada ya Kim kumwambia Khole kuwa wakiwa Dubai alikuwa na French kwa sekunde kumi tu.