Michezo
Fellipe Scorali afukuzwa kazi ya kuinoa timu ya Brazil
Kocha wa timu ya Taifa Brazil, Luiz Felipe Scolari amefukuzwa kazi ya ukocha katika kikosi hicho baada ya matokeo mabaya katika michuano ya Kombe la Dunia 2014.
Shirikisho la Soka la Brazil (CBF) limetangaza kuwa halita mwongezea mkataba mpya Luiz Felipe Scolari wa kuendelea kukinoa kikosi hicho kutokana na matokeo mabaya.
Scolari amelaumiwa kwa kushindwa kuiongoza Brazil iliyoambulia nafasi ya nne katika muchuano hiyo iliyoandaliwa nyumbani kwao huku ikishuhudia kombe likienda kwa Ujerumani.